2 Kings 2:2-6

2 aIlya akamwambia Al-Yasa, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.”

Lakini Al-Yasa akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja.

3 bWana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Al-Yasa na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?”

Al-Yasa akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”

4 cKisha Ilya akamwambia, “Baki hapa, Al-Yasa. Bwana amenituma Yeriko.”

Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko.

5Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Al-Yasa na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?”

Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.”

6 dKisha Ilya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.”

Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.

Copyright information for SwhKC