2 Kings 2:2-6
2 aIlya akamwambia Al-Yasa, “Kaa hapa. Bwana amenituma Betheli.” Lakini Al-Yasa akasema, “Kwa hakika, kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Kwa hiyo wakaenda Betheli pamoja. 3 bWana wa manabii waliokuwako huko Betheli wakamjia Al-Yasa na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Al-Yasa akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.” 4 cKisha Ilya akamwambia, “Baki hapa, Al-Yasa. Bwana amenituma Yeriko.” Naye akajibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wakaenda Yeriko. 5Wana wa manabii waliokuwako huko Yeriko wakamwendea Al-Yasa na kumuuliza, “Je, unajua ya kwamba Bwana atakuondolea bwana wako leo?” Akawajibu, “Ndiyo, najua, lakini msizungumze juu ya jambo hilo.” 6 dKisha Ilya akamwambia, “Kaa hapa. Bwana amenituma kwenda Yordani.” Naye akamjibu, “Kwa hakika kama Bwana aishivyo na wewe uishivyo, sitakuacha.” Hivyo wote wawili wakaendelea pamoja.
Copyright information for
SwhKC